• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Malalamiko na Mrejesho |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Malengo
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha & Biashara
      • Afya
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi & Zimamoto
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mazingira & Usafishaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • MIfugo & Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Water
    • Vitengo
      • TEHAMA & Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu.
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Ripoti Mbalimbali
      • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Wakulima Wa Pamba Serengeti Wahofia Mfumo Mpya Wa Ulipwaji wa fedha zao.

Imewekwa: May 29th, 2018

Wakulima wa pamba wilayani Serengeti wahofia mfumo mpya wa ulipaji wa pamba wakidai kuwa mfumo wa zamani ni bora zaidi.

Hayo yamesemwa kupitia viongozi wa vyama vikuu na vya msingi katika kikao kazi kilichofanyika jana Mei 28 2018 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

Wakitoa michango yao kwa nyakati tofauti Bwana Madaraka Gesura kutoka kikundi cha Nganyani A kilichopo katika Kijiji cha Wagete Kata ya Rigicha alisema kuwa wakulima wengi wa pamba wapo vijijini hivyo ni vyema wakilipwa huko huko kuliko kulipwa fedha zao kupitia akaunti za benki, huduma ambayo hutumia umbali mrefu kuifikia. Naye Bwana Julius Wanduku kutoka kikundi cha Nguvu moja kilichopo katika Kijiji cha Mosongo Kata ya Mosongo anasema kuwa mfumo mpya wa ulipaji ni kero kwa wakulima wadogo wa pamba ambao hupokea kiasi kidogo cha fedha ambayo ikipitia katika taasisi za fedha hukatwa, hivyo ni vyema wakulima wakilipwa pesa zao mkononi.

Katibu Tawala Wilaya ya Serengeti, Bwana Cosmas Quamara akifafanua jambo katika kikao kazi na Vyama vya Ushirika vya Pamba wilayani Serengeti.

Akitoa ufafanuzi wa hoja hizo za wakulima, Katibu Tawala wa Wilaya ya Serengeti Bwana Cosmas Quamara alisema kuwa Serikali imetoa mwongozo wa shughuli yote ya ukusanyaji na uuzaji wa pamba kutoka kwa wakulima, hivyo ni vyema wakazingatia maagizo yaliyotolewa na Serikali. Aidha kuhusu malipo ya fedha kupitia taasisi za fedha Bwana Quamara alisema kuwa ni vyema wakulima wakilipwa kupitia akaunti zao za benki huku akisema kuwa ni njia yenye usalama zaidi kwa fedha za wakulima

“Hapo nyuma tumekuwa tukiona wakulima wakidhulumiwa au kuibiwa fedha za mazao waliyouza, hivyo kupitia benki wakulima wanakuwa na usalama zaidi na fedha zao kwakuwa malipo yataingizwa moja kwa moja kwenye akaunti zao.” Alisema Bwana Quamara na kuendelea kwa kusema kuwa kuweka akiba katika taasisi za fedha kunapungua matumizi yasiyo na ulazima huku akiwasisitiza viongozi wa vyama hivyo kuongeza hamasa ili wakulima wengi wafungue akaunti katika taasisi za fedha huduma ambayo hutolewa bila gharama yoyote.

Katika kikao hicho vyama vikuu na vya msingi vilikabidhiwa mizani, vibao vya gredi ya pamba, stakabadhi na hati za malipo ili kufanikisha kazi ya ukusanyaji na uuzaji wa pamba.

Msimu wa ununuzi wa pamba wilayani Serengeti unatarajiwa kufunguliwa mapema mwezi Juni mwaka huu (2018) huku bei ya pamba ikitarajiwa kuwa ni Shilingi 1100 kwa kilo moja ya pamba ya gredi A na Shilingi 600 kwa kilo moja ya pamba ya gredi B.


MATUKIO KATIKA PICHA

Viongozi wa Vyama vya ushirikia vya Pamba wilayani Serengeti wakisikiliza jambo kwenye kikao.

Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Bi. Eliza Simon akitoa maelekezo ya uendeshaji wa zoezi la ukusanyaji wa pamba kwa Viongozi wa Vyama vya ushirika wilayani Serengeti

Mkaguzi wa Pamba kutoka Bodi ya Pamba Bwana Shabani Ramadhani akitoa maelekezo ya namna ya kutumia mizani kwa ajili ya upimaji wa pamba.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI KWA WAENDESHA BVR NA WAANDISHI MSAIDIZI April 28, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU. March 07, 2025
  • TANGAZO LA KUTOA MAONI KUHUSU SHERIA NDOGO. February 24, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA January 02, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU YA MALARIA WILAYANI SERENGETI

    April 25, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO WATEMBELEA ENEO LA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    April 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SERENGETI LAPITISHA BILIONI 48.8 KAMA MPANGO WA BAJETI YA HALMASHAURI 2025/2026.

    March 04, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI WILAYANI SERENGETI LAPITISHA MPANGO WA BAJETI YA TARURA BILIONI 2.4

    March 03, 2025
  • Angalia zote

Video

AKINA MAMA SERENGETI WASEMA ASANTE MAMA SAMIA.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Maktaba ya Picha za Matukio mbali mbali
  • Matokeo ya Kidato cha nne mwaka 2017
  • Bofya hapa kupata fomu mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • UCHAGUZI KIDATO CHA KWANZA 2022 SERENGETI DC
  • FOLLOW US INSTAGRAM
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili (FTNA) 2017
  • FOLLOW US TWITTER

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Rais
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Mkoa wa MARA
  • Tanzania National Parks TANAPA
  • Frankfurt Zoological Society (FZS)

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    31603 Stendi Kuu | Serengeti

    Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti

    Simu ya mezani: 0282985686

    Simu: 0782677763

    Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz

Other Contacts

   

Wageni waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti