Mahitaji ya maji kwa ajili ya binadamu na mifugo Wilaya ya Serengeti ni Mita za ujazo 42,438 kwa siku. Uwezo wa kutoa huduma hii kwa sasa ni Mita za ujazo 24,275 kwa siku, ambayo ni sawa na 58.68% ya mahitaji ya maji kwa Wilaya. Idadi ya kaya zinazopata huduma ya maji ndani ya Meta 400 ni 16,628 tu sawa na 40% ya kaya zote wilayani. Kaya 24,942 sawa na 60% ya kaya zote hupata huduma nje ya Meta 400.
Katika eneo la Mjini, Mamlaka ya Maji Mugumu (MUGUWASA) imeendelea kutoa huduma kwa wananchi ambapo kwa upande wa vijijini huduma imeendelea kutolewa kupitia ofisi ya Mhandisi wa maji Wilaya na kwa ngazi ya vijijini Kamati za maji ambazo ndivyo vyombo vya usimamizi zimeendelea kusimamia utoaji huduma.
31603 Stendi Kuu | Serengeti
Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti
Simu ya mezani: 0282985686
Simu: 0782677763
Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz
Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti