• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Malalamiko na Mrejesho |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Malengo
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha & Biashara
      • Afya
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi & Zimamoto
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mazingira & Usafishaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • MIfugo & Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Water
    • Vitengo
      • TEHAMA & Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu.
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Ripoti Mbalimbali
      • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WILAYA YA SERENGETI YAPATA MWENYEKITI MPYA WA HALMSAHURI

Imewekwa: December 11th, 2020

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti limemchagua Diwani wa Kata ya Busawe, Mhe. Ayubu Mwita  Makuruma kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2020 hadi 2025.

Uchaguzi  huo wa Mwenyekiti umefanyika Desemba 11, 2020 kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kwa kupiga kura za ndiyo au Hapana ambapo amepata kura zote 41 za ndiyo za Madiwani wateule 40 na  ya Mbunge wa Jimbo la Serengeti

Akizungumza baada ya kuchaguliwa na kuunda kamati za madiwani, Mhe. Ayubu Mwita  Makuruma (Mwenyekiti wa Halmashauri) amewashukuru madiwani kwa ushindi huo na kuwaahidi ushirikiano wa hali ya juu katika kushughulikia maendeleo ya wana-Serengeti.

“Nawaomba madiwani wenzangu tufanye kazi kwa bidii ili kuleta maendeleo kwa wananchi wetu wa Serengeti. Ninawaahidi kuwapa ushirikiano wa juu ili kuhakikisha Serengeti inapata maendeleo”

Makuruma ametumia nafasi hiyo pia kuwataka madiwani wote kushirikiana kwa karibu na viongozi wengine wakiwemo Mkuu wa Wilaya, Mbunge na Mkurugenzi wa Halmashauri katika kuwaondolea wananchi vikwazo vya maendeleo  kwa kuimarisha miundo mbinu kama barabara, ujenzi wa vyumba vya madarasa na vituo vya afya.


Katika zoezi hilo pia, Uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri umefanyika ambapo diwani wa Kata ya Kisangura, Mhe. Samson Ryoba Wambura (anayeongea - habari katika picha hapo chini)  amechaguliwa kwa kupata kura zote 41 za ndiyo


 (Makamu Mwenyekiti  wa halmashauri ya wilaya ya Serengeti Mhe. Samson Ryoba Wambura (Anayeongea hapo juu katika picha)


Mbunge wa Serengeti, Amsabi Mrimi , alipopata nafasi ya kuzungumza amesisitiza vipaumbele vitano vya kusaidia kuinua maendeleo ya Wilaya ya Serengeti

Amevitaja vipaumbele hivyo kuwa ni elimu na afya, utawala bora, mazingira na utalii, Miundo mbinu na uchumi. Amesisitiza kwa kusema kuwa Wanaserengeti tukishirikiana kwa pamoja tunaweza kuiboresha Serengeti na kuifanya jinsi tunavyotaka sisi kwa kusimamia hivyo vipaumbele vitano.

     Mbunge wa Serengeti, Amsabi Mrimi (aliyesimama) akizungumza katika kikao hicho


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA SERENGETI. June 11, 2025
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI KWA WAENDESHA BVR NA WAANDISHI MSAIDIZI April 28, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU. March 07, 2025
  • TANGAZO LA KUTOA MAONI KUHUSU SHERIA NDOGO. February 24, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WADAU WA ZAO LA TUMBAKU WATAKIWA KUZINGATIA MIONGOZO YA KILIMO CHA ZAO LA TUMBAKU ILI KUPATA TIJA YA ZAO HILO.

    June 17, 2025
  • WANANCHI WA KIJIJI CHA PARK NYIGOTI SERENGETI WANUFAIKA NA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI KUTOKA GRUMETI FUND.

    June 13, 2025
  • GRUMETI FUND YAENDELEA KUGUSA MAISHA YA VIJANA WA KIKE NA KIUME WILAYANI SERENGETI.

    June 04, 2025
  • SIKU YA MALARIA WILAYANI SERENGETI

    April 25, 2025
  • Angalia zote

Video

AKINA MAMA SERENGETI WASEMA ASANTE MAMA SAMIA.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Maktaba ya Picha za Matukio mbali mbali
  • Matokeo ya Kidato cha nne mwaka 2017
  • Bofya hapa kupata fomu mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • UCHAGUZI KIDATO CHA KWANZA 2022 SERENGETI DC
  • FOLLOW US INSTAGRAM
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili (FTNA) 2017
  • FOLLOW US TWITTER

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Rais
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Mkoa wa MARA
  • Tanzania National Parks TANAPA
  • Frankfurt Zoological Society (FZS)

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    31603 Stendi Kuu | Serengeti

    Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti

    Simu ya mezani: 0282985686

    Simu: 0782677763

    Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz

Other Contacts

   

Wageni waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti