• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Malalamiko na Mrejesho |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Malengo
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha & Biashara
      • Afya
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi & Zimamoto
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mazingira & Usafishaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • MIfugo & Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Water
    • Vitengo
      • TEHAMA & Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu.
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Ripoti Mbalimbali
      • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

SERENGETI YAZINDUA MKAKATI WA KUIMARISHA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI NGAZI YA ELIMU MSINGI

Imewekwa: September 23rd, 2022


 

Halmashauri ya wilaya ya Serengeti imezindua Rasmi Mkakati wa  kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji ngazi ya  elimu Msingi.Ambapo vitabu vitatu vilivyosheheni mikakati hiyo imezindulia na Katibu tawala Wilaya ya Serengeti Ndg.Qamaca C.Qamara, kwa Niaba ya Mkuu wa Wilaya  ya Serengeti.


Ikiwa ni  Takribani Mwezi Mmoja  tangu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa kuzindua mkakati huo kitaifa,na hatimaye kuzinduliwa hivi karibuni  kimkoa.

Akizinduza mikakati  hiyo wa niaba ya  Mkuu wa Wilaya ya Serengeti ,Katibu tawala Wilaya amewataka wadau hao waelimu kuzingatia yote yaliyokuwepo  kwenye mikakati hiyo ili kuweza kuleta ufaulu  na mabadiliko yanayotegemewa kitaifa.

Nae, afisa elimu sekondari  Mwl.Chatta luleka  Amesema kwamba Ofisi ya Rais – TAMISEMI yenye jukumu la kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa sera miongozo ya Elimu ya Msingi na Sekondari imetoa mikakati  ya kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji kwa ngazi ya Elimu Msingi ambapo Mkakati huo umegawanyika katika sehemu tatu, sehemu ya kwanza inaonesha mkakati wa kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji ngazi ya Elimu Msingi, sehemu ya pili  ni changamoto katika uboreshaji Elimu Msingi na Sekondari na hatua za kuchukua na sehemu ya tatu inaonesha uteuzi wa viongozi Elimu wa ngazi zote kuanzia katika shule hadi Mkoani.

Ameongeza pia  Lengo kuu la sehemu ya kwanza ya mkakati ni kuimarisha uandikishaji, ufundishaji na ujifunzaji ngazi ya Elimu Msingi.

‘’ Utekelezaji wa mkakati huo  unaongozwa na nadharia ya mabadiliko (Theory of change),  katika nadharia hiyo hatua ya kwanza ni kuchambua hali halisi ya tatizo ambalo huanza na viashiria vya tatizo, visababishi vya tatizo na athari za tatizo. Hatua ya pili ni kutafuta namna ya kukabili tatizo hilo kwa kuangalia fursa zilizopo katika mazingira ya fursa zilizopo mazingira ya tatizo ambazo zinaweza kutumika kutafuta tatizo husika. Hatua ya tatu ni kupanga mikakati ya kutumia fursa zilizopo kutatua tatizo ikiwa ni pamoja na kupanga utekelezaji wa mkakati, ufuatiliaji na  kufanya tathimini endelevu na tathimini tamati‘’Alisema Luleka

Aliongeza kwa kusema Sehemu ya pili ni uboreshaji wa Elimu Msingi na sekondari na hatua za kuchukua sehemu hii  inaonesha maboresho ya mifumo ya ufuatiliaji na usimamizi wa utoaji huduma yaliyofanywa, hali ya utoaji wa Elimu msingi na changamoto za uboreshaji wa Elimu na utatuzi wake na Sehemu ya tatu na ya mwisho ni uteuzi wa viongozi wa Elimu wa ngazi zote kuanzia ngazi ya shule, Kata, Halmashauri na Mikoa. Eneo hili limebainisha nafasi, sifa za kimuundo na kiutendaji, muundo wa kamati za mapendekezo ya uteuzi zitakavyofanya uchambuzi na kuwasilisha mapendekezo yake kwenye Mamlaka ya uteuzi.  Eneo hili lina sehemu tano, ambapo sehemu ya kwanza ni Mamlaka ya uteuzi wa viongozi, sehemu ya pili ni sifa za viongozi, sehemu ya tatu ni utaratibu wa uteuzi, sehemu ya nne ni uendeshaji wa kamati za mapendekezo ya uteuzi na sehemu ya tano ni majumuisho

Kuwepo kwa mkakati kutasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza na kundoa changamoto mbalimbali katika sekta ya elimu Msingi wilayani Serengeti.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI KWA WAENDESHA BVR NA WAANDISHI MSAIDIZI April 28, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU. March 07, 2025
  • TANGAZO LA KUTOA MAONI KUHUSU SHERIA NDOGO. February 24, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA January 02, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU YA MALARIA WILAYANI SERENGETI

    April 25, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO WATEMBELEA ENEO LA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    April 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SERENGETI LAPITISHA BILIONI 48.8 KAMA MPANGO WA BAJETI YA HALMASHAURI 2025/2026.

    March 04, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI WILAYANI SERENGETI LAPITISHA MPANGO WA BAJETI YA TARURA BILIONI 2.4

    March 03, 2025
  • Angalia zote

Video

AKINA MAMA SERENGETI WASEMA ASANTE MAMA SAMIA.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Maktaba ya Picha za Matukio mbali mbali
  • Matokeo ya Kidato cha nne mwaka 2017
  • Bofya hapa kupata fomu mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • UCHAGUZI KIDATO CHA KWANZA 2022 SERENGETI DC
  • FOLLOW US INSTAGRAM
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili (FTNA) 2017
  • FOLLOW US TWITTER

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Rais
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Mkoa wa MARA
  • Tanzania National Parks TANAPA
  • Frankfurt Zoological Society (FZS)

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    31603 Stendi Kuu | Serengeti

    Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti

    Simu ya mezani: 0282985686

    Simu: 0782677763

    Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz

Other Contacts

   

Wageni waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti