• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Malalamiko na Mrejesho |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Malengo
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha & Biashara
      • Afya
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi & Zimamoto
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mazingira & Usafishaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • MIfugo & Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Water
    • Vitengo
      • TEHAMA & Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu.
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Ripoti Mbalimbali
      • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Wakazi wa Robanda watakiwa kuchangamkia fursa za mikopo kujikwamua kiuchumi.

Imewekwa: February 4th, 2018

Mpango wa kurasimisha rasilimali na biashara za wanyonge Tanzania (Mkurabita) chini ya Ofisi ya Rais wakishirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti watoa mafunzo ya ujasiliamali kwa wananchi wa Kijiji cha Robanda kilichopo katika Kata ya Ikoma Wilayani Serengeti.

Mafunzo hayo yaliyojikita katika kujenga uwezo kwa wakulima na vyama vya wakulima yamefanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 1 mpaka 3 mwezi Februari 2018 katika ofisi za Kata yameonekena kutoa mwanga wa wananchi huku wakitakiwa kuchangamkia fursa za uwekezaji na kunufaika na mikopo kutoka taasisi za fedha.

Bwana Antony Temu ambaye ni meneja urasimishaji rasilimali ardhi vijijini kutoka MKURABITA anasema kuwa “Mafunzo haya yatawafungua wananchi juu ya fursa zilizopo hapa robanda na kuzitumia kujiongezea kipato” anaendela kwa kusema “Tuna lengo la kubadilisha mtazamo wa wakulima ili kuwa na kilimo endelevu chenye tija ndio maana tumezialika taasisi za fedha ili wapate elimu ya mikopo na kuona namna wanavyoweza kunufaika na mikopo hiyo”

Taasisi za fedha (benki) za NMB na CRDB zote kutoka Wilayani Serengeti zilipata nafasi ya kutoa mada kwa wananchi hao huku wakibanisha fursa walizonazo wananchi katika kuhifadhi fedha zao na kupata mikopo.

Bwana Edwin Costantine afisa mikopo kutoka benki ya CRDB anabainisha kuwa hati miliki ya kimila pekee haimwezeshi mtu kupata mikopo na kuwataka wananchi kutumia elimu waliyopata juu ya kuanzisha biashara, kutunza nyaraka na kuandaa maandiko mradi kuomba mikopo ambapo hati miliki hutumika kama dhamana ya mikopo hiyo. Huku Bwana Elvis Kokia afisa mikopo kutoka Benki ya NMB akisema kuwa lengo la taasisi za fedha katika kutoa mikopo ni kumsaidia mteja kutimiza malengo yake na sio kumpora hati yake baada ya kushindwa kurudisha fedha huku akiwasihi waombaji wa mikopo kuwa na malengo pindi wanapoomba mikopo kutoka taasisi za fedha.

Mzee Samson Wahika mkazi wa Kijiji cha Robanda hakusita kutoa maoni yake juu ya mafunzo hayo kwa kusema “Mafuzo haya yatanisaidia kwenda kuboresha shamba langu na kuliongezea thamani kwa kulima mazao ya biashara” aliendelea kwa kuomba mafunzo hayo yafike na sehemu nyingine Wilayani Serengeti na Taifa kwa ujumla ili wananchi wanufaike na rasilimali zao.

Katika mafunzo hayo ya siku tatu mada mbalimbali zilitolewa kutoka maafisa ardhi, kilimo, mifugo, maendeleo ya jamii pamoja na ushirika wote kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ambapo wananchi walielimishwa kuhusu umuhimu wa utunzaji wa nyaraka, elimu ya kilimo cha biashara, kuongeza thamani ya ardhi, kuandaa maandiko ya miradi pamoja na kudumisha vyama vya ushirika.

Aidha wananchi hao wametakiwa kuchangamkia fursa za mikopo kutoka Halmashauri kwa kuunda vikundi vya wanawake na vijana na kuwa na shughuli ya kiuchumi ili kuweza kupata mikopo kutoka Halmashauri.


MATUKIO KATIKA PICHA

Mwenyekiti wa Kijiji cha Robanda Mheshimiwa Mrobanda Japan akifungua mafunzo ua ujengaji uwezo kwa wakulima wa Kijiji cha Robanda.

Bwana Antony Temu Menejan urasimishaji rasilimali ardhi vijijini kutoka MKURABITA akitoa mada kwa wananchi wa robanda.

Afisa Ushirika Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Bi. Eliza Simon (aliyesimama) akitoa mafunzo kwa wananchi wa Kijiji cha Robanda.

Bwana Edwin Constantine afisa mikopo kutoka Benki ya CRDB Serengeti akitoa mada kwa wananchi wa Kijiji cha Robanda.

Bwana Elvis Kokia kutoka Benki ya NMb akitoa mada kwa wananchi wa Kijiji cha Robanda.

Mzee Samson Wahika mkazi wa Kijiji cha Robanda akisoma hati miliki ya kimila ya ardhi yake aliyopata baada ya urasimishaji wa ardhi yake.


Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI KWA WAENDESHA BVR NA WAANDISHI MSAIDIZI April 28, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU. March 07, 2025
  • TANGAZO LA KUTOA MAONI KUHUSU SHERIA NDOGO. February 24, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA January 02, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU YA MALARIA WILAYANI SERENGETI

    April 25, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO WATEMBELEA ENEO LA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    April 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SERENGETI LAPITISHA BILIONI 48.8 KAMA MPANGO WA BAJETI YA HALMASHAURI 2025/2026.

    March 04, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI WILAYANI SERENGETI LAPITISHA MPANGO WA BAJETI YA TARURA BILIONI 2.4

    March 03, 2025
  • Angalia zote

Video

AKINA MAMA SERENGETI WASEMA ASANTE MAMA SAMIA.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Maktaba ya Picha za Matukio mbali mbali
  • Matokeo ya Kidato cha nne mwaka 2017
  • Bofya hapa kupata fomu mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • UCHAGUZI KIDATO CHA KWANZA 2022 SERENGETI DC
  • FOLLOW US INSTAGRAM
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili (FTNA) 2017
  • FOLLOW US TWITTER

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Rais
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Mkoa wa MARA
  • Tanzania National Parks TANAPA
  • Frankfurt Zoological Society (FZS)

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    31603 Stendi Kuu | Serengeti

    Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti

    Simu ya mezani: 0282985686

    Simu: 0782677763

    Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz

Other Contacts

   

Wageni waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti