• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Malalamiko na Mrejesho |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Malengo
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha & Biashara
      • Afya
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi & Zimamoto
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mazingira & Usafishaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • MIfugo & Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Water
    • Vitengo
      • TEHAMA & Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu.
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Ripoti Mbalimbali
      • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MILIONI 120 KUKOPESHWA KWA VIKUNDI HAMSINI NA TANO

Imewekwa: December 10th, 2019

“Nyinyi vikundi hamsini na tano (55) mmeaminika, mmechujwa na mmeonekana kwamba mmekidhi vigezo ambavyo vimewekwa kwa ajili ya kupewa mikopo”

Hayo ni maneno ya Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mh. Nurdini Babu aliyekuwa mgeni rasmi wakati akifungua mafunzo kwa vikundi kuhusu namna ya kutumia kwa tija mikopo inayotolewa na serikali. Mafunzo yaliyofanyika leo tarehe 10/12/2019 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri

Babu amesema kuwa mikopo hiyo inayotolewa na serikali kupitia makusanyo ya halmashauri ipo na inawahusu wananchi wote ambao wapo tayari kujiunga kwenye vikundi vya uzalishaji mali pamoja na kukidhi masharti na taratibu za kuweza kupatiwa mkopo.

“Fedha hizi ni kwa mujibu wa sheria, lazima kwenye mapato ya ndani ya Halmashauri tutenge asilimia kumi (10%) kwa ajili ya vikundi mbalimbali, asilimia nne (4%) Wanawake, asilimia nne (4%) Vijana na asilimia mbili (2%) watu wenye Ulemavu”. Amesisitiza babu.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Mh. Juma Porini amesema kuwa serikali ya awamu ya tano chini ya Raisi Dr. John Magufuli imeondoa riba kwa vikundi vyote vinapochukua mkopo kutoka Halmashauri lengo likiwa ni kuwaondolea umasikini watanzania hasa wanawake, vijana na walemavu.

“Hatuchaji riba ya aina yoyote kwa hiyo hakuna hata mmoja asiyependa mkopo ambao hauna riba, kama ambavyo nyie mlipata hii fursa, iwe ni lazima na nyie kurudisha kwa wakati ili na wengine pia wapate hiyo fursa ya kukopa bila riba” Amesema Porini.

Image may contain: 5 people, including Juma Porini, people sitting

Mh. Porini akizungumza jambo

Awali akizungungumza wakati wa kutoa taarifa fupi kwa mgeni rasmi; Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya Bw. Wambura Sunday amesema kuwa mikopo hiyo hutolewa kwa vikundi ambavyo tayari vimeshatembelewa na kufanyiwa tathimini na kuona kuwa wanastahili kupewa mikopo, wanaelekezwa namna ya kufanya marejesho, elimu ya ujasiriamali pamoja na elimu ya kuweka na kukopa, na kwa sasa watatoa jumla ya Tshs. Milioni mia moja na ishirini (120,000,000) kwa vikundi vyote hamsini na tano.

Pia Wambura amewapongeza watumishi wa idara ya maendeleo ya jamii, watendaji kata na viongozi wa serikali za mitaa kwa kushirikiana kwa pamoja kusimamia vikundi na kuhakikisha vile vinavyokidhi vigezo ndivyo vinavyopatiwa mkopo ili viweze kuzalisha na kurejesha mikopo hiyo.

Kwa upande wao wanavikundi waliopata mafunzo hayo kutoka Halmashauri ya wilaya ya Serengeti wameishukuru serikali kwa kuwapatia mafunzo hayo na hatimaye kuwapa mkopo usiokuwa na riba na kusema kuwa wamefurahishwa na hatua hiyo na kwamba shughuli za vikundi hivyo zitafanyika kwa ufanisi baada ya mkopo huo usiokuwa na riba.

Aidha wameahidi kuirejesha mikopo hiyo mapema ili kuwapa nafasi wananchi wengine waweze kukopa.

Image may contain: one or more people, people sitting, crowd and indoor


Image may contain: 2 people, people sitting, table and indoor

Wanavikundi mbalimbali wakisikiliza maelekezo kwa makini

Katika robo hii ya kwanza ya mwaka wa fedha 2019/2020 jumla ya Vikundi hamsini na tano (55) vinatarajiwa kupewa jumla ya Tshs. Milioni mia moja na ishirini (120,000,000) kutoka katika asilimia 10 ya makusanyo ya mapato ya ndani ya Halmashauri ikiwa vikundi thelatini vya wanawake (Tshs. Milioni sitini), vikundi kumi na tisa vya vijana (Tshs. Milioni hamsini) na vikundi sita vya watu wenye ulemavu (Tshs. Milioni kumi) vitanufaika na mkopo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ili kuwaongezea wananchi husika uwezo wa kujiongezea kipato na kurejesha fedha hizo bila riba ili ziweze kuwasaidia wengine kuinuka kiuchumi.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI KWA WAENDESHA BVR NA WAANDISHI MSAIDIZI April 28, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU. March 07, 2025
  • TANGAZO LA KUTOA MAONI KUHUSU SHERIA NDOGO. February 24, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA January 02, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU YA MALARIA WILAYANI SERENGETI

    April 25, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO WATEMBELEA ENEO LA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    April 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SERENGETI LAPITISHA BILIONI 48.8 KAMA MPANGO WA BAJETI YA HALMASHAURI 2025/2026.

    March 04, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI WILAYANI SERENGETI LAPITISHA MPANGO WA BAJETI YA TARURA BILIONI 2.4

    March 03, 2025
  • Angalia zote

Video

AKINA MAMA SERENGETI WASEMA ASANTE MAMA SAMIA.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Maktaba ya Picha za Matukio mbali mbali
  • Matokeo ya Kidato cha nne mwaka 2017
  • Bofya hapa kupata fomu mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • UCHAGUZI KIDATO CHA KWANZA 2022 SERENGETI DC
  • FOLLOW US INSTAGRAM
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili (FTNA) 2017
  • FOLLOW US TWITTER

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Rais
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Mkoa wa MARA
  • Tanzania National Parks TANAPA
  • Frankfurt Zoological Society (FZS)

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    31603 Stendi Kuu | Serengeti

    Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti

    Simu ya mezani: 0282985686

    Simu: 0782677763

    Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz

Other Contacts

   

Wageni waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti