• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Malalamiko na Mrejesho |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Malengo
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha & Biashara
      • Afya
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi & Zimamoto
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mazingira & Usafishaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • MIfugo & Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Water
    • Vitengo
      • TEHAMA & Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu.
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Ripoti Mbalimbali
      • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MH. RYOBA ALIA NA MABOMA

Imewekwa: August 16th, 2019

Mbunge wa Jimbo la Serengeti Mh. Marwa Ryoba amewataka wananchi na wadau wote wa maendeleo Wilayani Kuhakikisha kuwa wanajenga Maboma ili Serikali Kuu nayo iweze kuchangia katika miradi mbali mbali.

Mh. Ryoba ameyasema hayo leo Katika Kijiji cha Kitunguruma kilichopo Kata ya Mbalibali wakati wa ziara ya wajumbe wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ilipokuwa ikitembelea miradi mbalimbali ambayo miradi mingi fedha zake zinatokana na mpango wa lipa Kulingana na matokeo (P4R), Halmashauri pamoja na nguvu za wananchi

Bweni la wavulana katika shule ya sekondori Ngoreme likiwa bado halijakamilika

Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango hufanya ziara zake za kutembelea miradi ya maendeleo kwa mujibu wa kanuni za kamati za kudumu za Halmashauri na lengo kuu pamoja na mambo mengine ni kuona na kutathimini thamani ya fedha pale ilipotekelezwa, kushauri na kuhamasisha jamii katika kuchangia miradi ya maendeleo.

Moja ya darasa katika Shule ya sekondari Nyansurura

Akizunguza mara baada ya kamati hiyo kukagua ukamilishaji wa madarasa matano katika Shule ya Sekondari Kitunguruma Mh. Ryoba amewataka wananchi na wadau wote kuhakikisha kuwa wanajitahidi kujenga majengo mengi wawezavyo ili Serikali Kuu nayo iweze kuchangia fedha kwa wingi.

Akitolea mfano Shule ya Kitunguruma ndio shule iliyopewa fedha nyingi kati ya Milioni mia tatu zilizopokelewa katika wilaya nzima kwani shule hiyo ilipewa Milioni Hamsini na hii ni kutokana na kuwa na maboma manne.

Baadhi ya madarasa katika shule ya sekondari Kitunguruma

Hivyo aliwasisitiza wananchi na wadau wote wa maendeleo kuhakikisha wanajenga maboma ya kutosha na amesema kuwa serikali imetenga na inategemea kuletea fedha nyingine kabla ya kuvunja kwa bunge tukufu.

Shule mpya inayoendelea kujengwa katika kijiji cha Musati Kata Kibanchebanche

Kamati Hii iliweza kutembelea miradi mbalimbali ambayo ni

  • Mradi wa Ujenzi wa nyumba ya walimu “Six in One” shule ya sekondali Natta
  • Ukamilishaji wa maboma mawili ya vyumba vya madarasa shule ya sekondari Nagusi
  • Ukamilishaji wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya Sekondari Mama maria nyerere
  • Ujenzi wa shule ya Msingi Kemgongo na ofisi ya walimu
  • Ukamilishaji wa maboma mawili ya vyumba vya madarasa shule ya sekondari Dr. Omari Ali Juma
  • Ujenzi wa shule ya msingi Kemalambo Kwa tumia fedha za mapato ya ndani
  • Ujenzi wa shule mpya Kata ya Kibanchebanche
  • Ukamilishaji wa maboma matano ya vyumba vya madarasa shule ya sekondari Kitunguruma
  • Ukamilishaji wa vyumba viwili vya madarasa shule ya sekondari Machochwe
  • Ujenzi wa chumba kimoja cha darasa shule ya msingi Nyamakendo
  • Ukamilishaji wa vyumba viwili vya madarasa shule ya sekondari Nyansurura
  • Ukamilishaji wa vyumba viwili vya madarasa shule ya sekondari Busawe na
  • Ujenzi wa Bweni la Wavulana Shule ya sekondari Ngoreme

Nyumba ya walimu "Six in one" katika Shule ya sekondari Natta

Wakati huo huo Mh. Ryoba amewaahidi watumishi wa Kata ya Busawe, Kenyamonta na Majimoto kwanunulia Jezi na Mpira wa miguu mmoja moja kwa kila kata hizo aidha amesema kuwa anafikiria kuanzisha ligi ya mpirta kbla ya mwezi Disemba mwaka huu huku akifikiria kuwa mshindi wa kwanza atapatiwa zawadi ya fedha Taslimu Milioni Moja na Mshindi wa pili fedha Taslimu laki sita na uku akisema mshindi watatu watapanga

Aliyasema hayo wakati akiwasalimia watumishi wa kata hizo waliokuwa wakifanya mazoezi katika uwanja wa michezo uliopo katika shule ya sekondari ya Ngoreme iliyopo katika Kata ya Kenyamonta.


Mh. Mbunge (Mwenye suti ya Bluu) pamoja na baadhi ya wajumbe wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wachezaji watumishi kata ya Busawe, Kenyemonta na Majimoto

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI KWA WAENDESHA BVR NA WAANDISHI MSAIDIZI April 28, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU. March 07, 2025
  • TANGAZO LA KUTOA MAONI KUHUSU SHERIA NDOGO. February 24, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA January 02, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU YA MALARIA WILAYANI SERENGETI

    April 25, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO WATEMBELEA ENEO LA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    April 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SERENGETI LAPITISHA BILIONI 48.8 KAMA MPANGO WA BAJETI YA HALMASHAURI 2025/2026.

    March 04, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI WILAYANI SERENGETI LAPITISHA MPANGO WA BAJETI YA TARURA BILIONI 2.4

    March 03, 2025
  • Angalia zote

Video

AKINA MAMA SERENGETI WASEMA ASANTE MAMA SAMIA.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Maktaba ya Picha za Matukio mbali mbali
  • Matokeo ya Kidato cha nne mwaka 2017
  • Bofya hapa kupata fomu mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • UCHAGUZI KIDATO CHA KWANZA 2022 SERENGETI DC
  • FOLLOW US INSTAGRAM
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili (FTNA) 2017
  • FOLLOW US TWITTER

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Rais
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Mkoa wa MARA
  • Tanzania National Parks TANAPA
  • Frankfurt Zoological Society (FZS)

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    31603 Stendi Kuu | Serengeti

    Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti

    Simu ya mezani: 0282985686

    Simu: 0782677763

    Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz

Other Contacts

   

Wageni waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti