• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Malalamiko na Mrejesho |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Malengo
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha & Biashara
      • Afya
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi & Zimamoto
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mazingira & Usafishaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • MIfugo & Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Water
    • Vitengo
      • TEHAMA & Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu.
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Ripoti Mbalimbali
      • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

GRUMETI FUND BEGA KWA BEGA NA WASICHANA SERENGETI,YAWAHIMIZA KUJILINDA KUZIFIKIA NDOTO ZAO

Imewekwa: March 26th, 2023


KAMPUNI ya Grumeti Fund kupitia Idara yake ya Maendeleo ya Jamii imeendelea kutoa semina kwa vijana wakiume na wakike Wilayani Serengeti na Bunda ambapo mpaka sasa imefikia mabinti 9,308 na vijana wa kiume 1,018 kuanzia 2017- 2022.

Katika semina hizo mabinti 9,308 kutoka Sekondari 19 za Wilaya ya Bunda na Serengeti, walipewa taulo za kike za kutumia kwa muda wa mwaka mmoja na miezi sita (reusable pads).

Katika kongamano hilo lilofanyika Mwanzoni Mwa wiki Hii, vijana wa kike wameaswa kujituma na kuepuka vishawishi ili kutimiza ndoto zao na kuwa msaada katika Taifa huku ikitoa taulo za kike 761 zinazoweza kufuliwa na kudumu kwa muda wa mwaka mmoja na nusu kwa wasichana wote 761 waliohudhuria semina hiyo.

Akizungumza na wasichana hao katika kongamano hilo, Mgeni rasmi Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Neema Msuya ameipongeza kampuni ya Grumeti Fund kwa kuona umuhimu wa kufanya makongamo hayo na kuwataka wasichana hao kutekeleza yote waliyojifunza ili kutimiza ndoto zao.


"Nawashukuru sana Grumeti Fund, tunatumaini kwa juhudi za wadau hawa  hakutuwa na utoro mashuleni, mimba za utotoni, ndoa za mapema na ukeketaji.


"Nyinyi mpo kwenye safari ya maisha, safari bado ni ndefu mkawe na ujasiri, uthubutu, mjiamini mkawe watu bora" amesema Neema

Aidha, ametoa wito kwa mashirika, kampuni na taasisi nyingine kuiga mfano wa Grumeti Fund katika kuendesha semina na makongamano ya kufundisha vijana wa kiume na wakike katika maeneo mbalimbali ili kuwasaidia katika maisha yao.


"Grumeti Fund, naomba muendelee kuwa chachu ya mabadiliko na maendeleo katika Wilaya yetu ya Serengeti na Taifa kwa ujumla" amesema Neema.

Kongamani hilo  limehusisha wasichana kutoka shule za Sekondari Issenye, Nagusi,na Rigicha za wilayani Serengeti.


Aidha, amewataka wasichana hao kujituma kielimu  na kiujasiriamali ili kutimiza ndoto zao  kwa sababu ya uwepo wa mazingira rafiki na  amewasihi kumtanguliza Mwenyezi Mungu katika maisha yao na kuepuka makundi hatarishi na tamaa.


Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii  Grumeti Fund, Frida Mollel amewakumbusha wasichana hao kuwa wana haki ya kusema hapana kwa mila na desturi potofu ambazo zinawakandamiza na kuwapotezea fursa mbalimbali za kimaisha ikiwemo masomo.


 Ameongeza pia:

 ‘’Mwanamke au binti unanafasi kubwa sana katika jamii kufanya mabadiliko ya kiuchumi, kielimu, na kisayansi’’

Frida amewasisitiza mabinti kuwa wanaweza kufanya chochote na kuwa mtu yeyote na  kutimiza ndoto walizonazo, ikiwa watasimama kidete kusimamia maisha yao na kuacha kukumbatia vitu vinavyokwamisha ndoto zao ikiwemo mimba zisizotarajiwa, makundi rika, utoro, ndoa za utotoni na kupoteza muda kwenye mitandao ya kijamii.


Lakini pia ametoa wito kwa wazazi kuunga mkono juhudi za Serikali off kwa kuchangia katika  ujenzi wa miundombinu mbalimbali yakiwemo madarasa na mabweni ili kuboresha elimu zaidi na kufanya watoto kuwa salama.


Grumeti Fund hualika wadau mbalimbali kutoka katika asasi za kijamii ili kuzungumza na mabinti katika maeneo mbalimbali ya maisha yao wakati wa kongamano.


 Kwa upande wake, Mkufunzi wa Chuo cha  Sayansi za afya Kisare, Mwl.Restuda Murutta amewataka wasichana hao kuepuka ndoa za utotoni, mimba zisizotarajiwa na kudumisha usafi haswa kipindi cha hedhi.



‘’Tujifunze kujitunza ili kuepuka mimba za utotoni ili kuepuka madhara yatokanayo na kubeba mimba mapema, lakini pia tukumbuke kuweka mazingira yetu ya choo safi ili tusipate magonjwa.’’alisema Mwl Restuda


Nae, Mkurugenzi wa kituo cha nyumba Salama, Hope for Girls and women in Tanzania, Rhobi Samweli ametoa wito kwa wasichana  hao kupinga ukeketaji na kuwa chachu ya mabadiliko  kwa kuielimisha jamiii juu ya madhara ya ukeketaji na kutoa taarifa ya vitendo vya ukeketaji,


Kupitia Kongamano hilo Wasichana hao walipata wasaa wakuwasilisha changamoto wanazopitia ikiwa ni pamoja na kutoa maoni yao ya namna changamoto hizo zinavyoweza kutatuliwa. Changamoto hizo ni pamoja na ndoa za utotoni, ukatili wa kijinsia  kama ukeketaji, kunyimwa haki ya elimu, vishawishi, mila na desturi potofu na kubaguliwa.


Grumeti Fund imekuwa ikitoa ufadhili wa kimasomo kwa vijana, elimu ya ujasiriamali na mazingira kwa jamii pamoja na uhifadhi wa wananyama pori.


Mwisho.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI KWA WAENDESHA BVR NA WAANDISHI MSAIDIZI April 28, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU. March 07, 2025
  • TANGAZO LA KUTOA MAONI KUHUSU SHERIA NDOGO. February 24, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA January 02, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU YA MALARIA WILAYANI SERENGETI

    April 25, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO WATEMBELEA ENEO LA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    April 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SERENGETI LAPITISHA BILIONI 48.8 KAMA MPANGO WA BAJETI YA HALMASHAURI 2025/2026.

    March 04, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI WILAYANI SERENGETI LAPITISHA MPANGO WA BAJETI YA TARURA BILIONI 2.4

    March 03, 2025
  • Angalia zote

Video

AKINA MAMA SERENGETI WASEMA ASANTE MAMA SAMIA.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Maktaba ya Picha za Matukio mbali mbali
  • Matokeo ya Kidato cha nne mwaka 2017
  • Bofya hapa kupata fomu mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • UCHAGUZI KIDATO CHA KWANZA 2022 SERENGETI DC
  • FOLLOW US INSTAGRAM
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili (FTNA) 2017
  • FOLLOW US TWITTER

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Rais
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Mkoa wa MARA
  • Tanzania National Parks TANAPA
  • Frankfurt Zoological Society (FZS)

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    31603 Stendi Kuu | Serengeti

    Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti

    Simu ya mezani: 0282985686

    Simu: 0782677763

    Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz

Other Contacts

   

Wageni waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti