KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO ikiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Serengeti Mhe. Ayub Makuruma ambaye pia ni Diwani wa kata ya Busawe,ilifanya Ziara katika Hospitali ya Wilaya ya Serengeti kwaajili ya kutembelea na kukagua Ukamilishaji wa Wodi ya Wazazi Kibeyo(Maternity block),Ambayo ilianza kujengwa mwezi desemba 2021 ikiwa ni muendelezo wa Ujenzi wa Hospitali.Mradi huu umegharimu kiasi cha Jumla ya Tsh.130,395,000/=
Jengo hili linasehemu Kuu tano ambazo ni sehemu ya Kulaza Wajawazito kabla ya Kujifungua(Antenatal),Sehemu ya kujifungulia (Labor Ward),Sehemu ya kufanyia Upasuaji (Theatre),Chumba cha watoto Njiti (Kangoro Room),Sehemu ya kulaza akina mama baada ya kujifungua (Postnatal).Kukamilika Kwa mradi utakuwa na uwezo wa Kulaza akina mama 40 kwa wakati Mmoja.
Mradi huu mpaka sasa umefikia hatua ya kufunga Lenta na kujenga kozi mbili za juu ili kuruhusu hatua ya kupaua kuendelea.
Akizungumza wakati wa Ukaguzi wa Mradi huo Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Serengeti Mhe.Ayub Makuruma amemshukuru Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Sami Suluhu Hassani kwa kutoa Fedha nyingi za miradi katika halmashauri ya Wilaya ya Serengeti pia amempongeza Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Kibeyo kwa usimamizi mzuri wa mradi huo,aidha kamati imeutaka uongozi wa hospitali kusimamia Ujenzi na kuhakikisha una kamilika kwa wakati ili uweze kuwasaidia wananchi.
Awali Mganga Mkuu Wilaya Dkt. Emilliana Donald akisoma taarifa ya ujenzi wa wodi kwa Kamati ya Uongozi na Mipango amesema katika Kukamilisha mradi huu wamepitia changamoto mbalimbali zikiwemo mfumo wa bei uliopelekea kupanda kwa gharama za vifaa vya Ujenzi.
31603 Stendi Kuu | Serengeti
Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti
Simu ya mezani: 0282985686
Simu: 0782677763
Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz
Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti