Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Serengeti Mhe.Samson R. Wambura ambaye pia ni Diwani wa kata ya Kisangura , Tarehe 31.10.2022 imefanya Ziara ya Kukitembelea na kushuhudia Miradi inayofanywa na Kikundi cha Neema kilichopo kata ya Morotonga.
Kikundi hiki kilianzishwa mwaka 2008,kikiwa na idadi ya wanachama 30 kwa ajili ya kuweka fedha na kukopeshana mpaka sasa kikundi hiki kina wanachama walio hai 20.
Dhumuni la kikundi hiki ni kuwainua akina mama katika miradi midogo midogo ili kuweza kuboresha masiha ya familia zao na kukuza vipato,Kufikia lengo hilo kikundi kimeanzisha miradi ya kutengeneza sabuni za maji na za vipande ,kuuza vitenge na mabaitiki,kufuga kuku wa kienyeji ,shamba dogo la migomba na ushonaji wa mikeka.
Kikundi hiki ni miongoni mwa vikundi vilivyopo katika halmashauri ya wilaya ya Serengeti ambacho pia kinanufaika na mikopo ambapo mpaka sasa kikundi kishakopeshwa jumla ya Tsh.6,000,000/=
Kikundi hiki kinapitia changamoto ya kukosa masoko kwa ajili ya kuuza bidhaa zao.
Kamati imekipongeza kikundi hicho na kukitaka kiiendelee kufanya kazi kwa juhudi na kujitahidi kutafuta masoko katika maeneo mbalimbali ikiwemo minadani ili kuweza kuuza bidhaa zao kwa haraka
31603 Stendi Kuu | Serengeti
Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti
Simu ya mezani: 0282985686
Simu: 0782677763
Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz
Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti