Taasisi ya Worldchanger Vision iliyopo wilayani Serengeti Mkoa Wa Mara,imeendelea kugusa na kurejesha matumaini ya kielimu kwa watoto wengi wilayani Serengeti ambao wapo katika mazingira magumu na yanayokatisha tamaa kuendelea na Elimu.
Katika kutambua umuhimu na faida kubwa iliyopo katika kuwekeza katika elimu haswa kwa watoto taasisi hii imejikita katika kuhakikisha watoto wote wanapata elimu sawa na wale ambao wapo katika mazingira mazuri.
Taasisi hii yenye chuo cha ufundi wilayani Serengeti imekuwa na manufaa kwa vijana wengi wilayani hapa na kusadia watoto hao kupat Ujuzi na hatimaye kuweza kujiajiri.
Familia ya Ndg.Makuru chacha,kupitia kitengo cha ustawi wa Jamii cha wilaya ya Serengeti, imeweza kuguswa na shirika hili na kuwezesha watoto wa 5 wa familia hiyo kupata mahitaji yote ya shule ili waweze kurejea shuleni baada ya kukwama kuendelea ana masomo baada ya kukosa mahitaji muhimu.
‘’ili kupata madaftari na sare za shule za mimi na wadogo zangu ilipasa nifanye nifanye kazi kwa juhudi kwani baba angu hajiwezi ni mlemavu,ulemavu alioupata kutoka na kukanyagwa na tembo akiwa shambani na hivyo kumfanya kupata ulemavu wa kudumu na mama yetu alikimbia familia miaka mingi iliyopita,hivyo nikiwa kijana mkubwa wa familia hii inanipa kupambana ili kuilea familia’’alisema mwita
Pamoja na jitahada za mtoto huyu bado hakufanikiwa kufanikisha mahitaji yake na wadogo zake hivyo ikamfanya kufika ofisi za ustawi wa jamii na kupitia Mdau World changer kupata msaada huo.
Aidha,idara kupitia wadau wake tasisi ya worldchanger vision iliwashika mkono watoto hawa na kuwawezesha kwa mahitaji yote ya shule na hivyo kurejea shuleni kuendelea na masomo.
Kwa upande wa Mratibu wa Taasisi ya Worldchanger vision Ndg.Sulus Samweli Akitoa msaada wa vifaa vya shule kwa watoto hao kwa niaba ya Taasisi hiyo amemuomba mlezi wa watoto hao kuhakikisha anawahimiza watoto hao kuhudhuria masomo kwa kuwasimamia kwa ukaribu kwa na wameahidi kama taasisi wataendelea kuwafaatilia kwa ukaribu ili watimize ndoto zao.
Kupitia ushirikiano huu kati ya serikali na wadau ni chachu kubwa ya kuondoa changamoto zilizopo katika sekta ya elimu,hivyo kuondoa watu wasiojua kusoma na kuandika katika Jamii.
Tunawashukuru na kuipongeza Taasisi ya WCV Kwa kuonesha upendo wa Hali ya Juu kwa kuwa Msaada kwa Jamii ya Serengeti haswa Watoto.
31603 Stendi Kuu | Serengeti
Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti
Simu ya mezani: 0282985686
Simu: 0782677763
Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz
Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti