• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Malalamiko na Mrejesho |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Malengo
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha & Biashara
      • Afya
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi & Zimamoto
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mazingira & Usafishaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • MIfugo & Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Water
    • Vitengo
      • TEHAMA & Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu.
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Ripoti Mbalimbali
      • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Shilingi Bilioni sita kuziunganisha Serengeti na Tarime

Imewekwa: January 18th, 2018

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali inayo fedha kiasi cha bilioni sita za kitanzania katika ujenzi wa daraja la mto mara linalojengwa katika mpaka wa Wilaya ya Serengeti na Tarime.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Serengeti Mheshimiwa Marwa Ryoba Mara baada ya kuwasili Wilayani Serengeti akitokea Wilaya ya Tarime

Mheshimiwa Majaliwa amsema hayo leo tarehe 18 januari 2018 wakati akiwa katika ziara ya kikazi katika Mkoa wa Mara alipokuwa anaingia katika Wilaya ya Serengeti akitokea Wilaya ya Tarime ambako Mto Mara hutenganisha Wilaya hizo.

“Tunatarajia ifikapo mwezi wa tatu mwaka huu (2018) daraja hili litakuwa limeshakamilika hivyo kurahishisha huduma za mawasiliano kati ya wilaya hizi kwa ufanisi zaidi "alisema Mheshimiwa Majaliwa.

Kukamilika kwa daraja hilo lililoanza kujengwa mwezi wa tatu (3) mwaka 2017  na mkandarasi Gemen Engineering kunaashiria ujio wa barabara ya lami kutoka Tarime mpaka Mji wa Mugumu Serengeti na kuondoka kero ya muda mrefu ya wakazi wa Mji wa Mugumu Serengeti wanaokosa huduma muhimu ya mawasilano ya barabara ya lami inayounganisha na Wilaya hiyo na zingine.

Mheshimiwa Majaliwa alisema kuwa baada ya ujenzi wa daraja kukamilika, serikali itaanza mara moja mchakato wa ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka tarime mpaka Mji wa Mugumu. Waziri Mkuu hakusita kuzungumzia kero ya muda mrefu juu ya barabara ya lami inayounganisha Mkoa wa Mara na Arusha kupitia Wilaya ya Serengeti na Ngorongoro na kusema “kwa muda mrefu sasa serikali imekuwa katika mazungumzo na wadau wa maendeleo wa kimataiafa  juu ya ujenzi wa barabara ya lami katika hifahdi ya taifa ya Serengeti ambayo ni miongoni wa vivutio vya dunia na kulingana na makubaliano tuliyowekeana bado ipo changamoto katika fumbuzi wa jambo hili” alisema Mheshimiwa Majaliwa  na kuwataka wananchi kuwa na subira wakati serikali ikitafuta ufumbuzi wa jambo hilo.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Mheshimiwa Juma Porini wakati anawasili katika Wilaya ya Serengeti akitokea Wilaya ya Tarime.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Mhandisi Juma Hamsini wakati akiwasili Wilaya ya Serengeti akitokea Wilaya ya Tarime.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA SERENGETI July 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA SERENGETI. June 11, 2025
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI KWA WAENDESHA BVR NA WAANDISHI MSAIDIZI April 28, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU. March 07, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SEMINA YA SIKU TATU KWA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA JIMBO LA SERENGETI YAHITIMISHWA RASMI.

    August 06, 2025
  • BARAZA LA MAMLAKA YA MJI MDOGO SERENGETI LAZINDULIWA LEO.

    July 10, 2025
  • TSC SERENGETI YAENDESHA MAFUNZO ELEKEZI KWA WALIMU WAPYA 89.

    July 09, 2025
  • DAS MASIKO AKABIDHIWA OFISI.

    July 04, 2025
  • Angalia zote

Video

AKINA MAMA SERENGETI WASEMA ASANTE MAMA SAMIA.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Maktaba ya Picha za Matukio mbali mbali
  • Matokeo ya Kidato cha nne mwaka 2017
  • Bofya hapa kupata fomu mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • UCHAGUZI KIDATO CHA KWANZA 2022 SERENGETI DC
  • FOLLOW US INSTAGRAM
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili (FTNA) 2017
  • FOLLOW US TWITTER

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Rais
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Mkoa wa MARA
  • Tanzania National Parks TANAPA
  • Frankfurt Zoological Society (FZS)

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    31603 Stendi Kuu | Serengeti

    Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti

    Simu ya mezani: 0282985686

    Simu: 0782677763

    Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz

Other Contacts

   

Wageni waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti