• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Malalamiko na Mrejesho |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Malengo
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha & Biashara
      • Afya
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi & Zimamoto
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mazingira & Usafishaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • MIfugo & Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Water
    • Vitengo
      • TEHAMA & Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu.
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Ripoti Mbalimbali
      • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

SERENGETI YATOA MIKOPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA MILIONI 136/-

Imewekwa: January 13th, 2023

      


Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti mkoani Mara imetoa mkopo usio na riba yenye kiasi cha Tsh. Milioni 136,374,130/-  kwa vikundi 28 vya wanawake,vijana na watu wenye walemavu ikiwa ni mkopowa wa asilimia 10% za makusanyo  kwa robo  ya pili ya mwaka wa fedha 2022/2023.


Akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi  hundi ya mfano  ,Mhe.Ayubu Makuruma , Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Serengeti ametoa wito kwa vikundi hivyo kutumia fursa ya mikopo isiyo na riba inayotolewa na  Halmashauri ili  kujikwamua kiuchumi ambapo amesisitiza vikundi hivyo kurejesha mikopo hiyo kwa wakati  ili kuendelea kunufaika zadi na kutoa wigo wa utoaji wa mikopo kwa wananchi wengine.


‘Natoa wito kwenu baada ya kupata mkopo huu fanyeni kazi kwa bidi ili mjikwamue kiuchumi sambamba na kurejesha kwa wakati kwa mujibu wa utaratibu kwani hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wale wasio fanya marejesho na kukwamisha wananchi wengine  kunufaika ‘’amesema Makuruma.

Katibu tawala wa  wilaya ya Serengeti Ndg.Qamara C.Qamara  kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Serengeti amevisisitiza vikundi vilivyonufaika na mkopo huo kutumia mkopo  huo kwa malengo na  shughuli zilizokusudiwa ili kujikwamua kiuchumi.

‘’Niwasihi  mzingatie yote tuliyowaasa,Nendeni Mkaweke juhudi  kulingana na malengo ya vikundi vyenu tunataka tuone tija’’amehimiza  Qamara.

Mwakilishi  wa meneja wa Benki ya NMB Bi.Beatrice Kamugisha ametoa wito kwa vikundi kuzitumia pesa hizo vizuri kwa manufaa yao na taifa kwa ujumla lakini pia kujiwekea akiba .


Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya Serengeti Ndg.Kivuma H.Msangi amevipongeza vikundi vya wanawake kwa kuwa mstari wa mbele katika kurejesha mikopo hiyo na kuvitaka vikundi vya vijana na watu wenye ulemavu kuongeza juhudi katika urejeshaji wa mikopo sambamba na kufuata taratibu stahiki wakati urejesha wa mikopo hiyo.


Naye Katibu wa mbunge Ndg. Julius Anthony kwa niaba ya Mbunge amehimiza  vikundi vilivyonufaika   kuendelea kukuza mitaji   kwa kujikita katika shughuli mbalimbali za kiuchumi pia ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Serengeti kwa juhudi kubwa ya ukusanyaji wa mapato na utoaji wa asimilia 10% kwenye vikundi.


Awali akisoma taarifa kwa Mgeni Rasmi afisa wa Maendeleo ya Jamii kwa niaba ya mkuu wa Idara hiyo Bi.Neema Msuya amesema mkopo huo  Milioni 136,374,130/- ni muendelezo wa utoaji wa mikopo isiyo na riba inayotolewa na halmashauri  ambapo mkopo wa

million. 152,460,000/- kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Kupitia mkopo huo vikundi 17 vya wanawake,vinane (8) na vitatu (3) vya watu wenye ulemavu vilinufaika na mkopo huo.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na  wakuu wa idara na vitengo, na watumishi wa idara ya maendeleo ya jamii wa halmashauri ya wilaya ya Serengeti.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI KWA WAENDESHA BVR NA WAANDISHI MSAIDIZI April 28, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU. March 07, 2025
  • TANGAZO LA KUTOA MAONI KUHUSU SHERIA NDOGO. February 24, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA January 02, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU YA MALARIA WILAYANI SERENGETI

    April 25, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO WATEMBELEA ENEO LA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    April 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SERENGETI LAPITISHA BILIONI 48.8 KAMA MPANGO WA BAJETI YA HALMASHAURI 2025/2026.

    March 04, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI WILAYANI SERENGETI LAPITISHA MPANGO WA BAJETI YA TARURA BILIONI 2.4

    March 03, 2025
  • Angalia zote

Video

AKINA MAMA SERENGETI WASEMA ASANTE MAMA SAMIA.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Maktaba ya Picha za Matukio mbali mbali
  • Matokeo ya Kidato cha nne mwaka 2017
  • Bofya hapa kupata fomu mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • UCHAGUZI KIDATO CHA KWANZA 2022 SERENGETI DC
  • FOLLOW US INSTAGRAM
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili (FTNA) 2017
  • FOLLOW US TWITTER

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Rais
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Mkoa wa MARA
  • Tanzania National Parks TANAPA
  • Frankfurt Zoological Society (FZS)

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    31603 Stendi Kuu | Serengeti

    Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti

    Simu ya mezani: 0282985686

    Simu: 0782677763

    Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz

Other Contacts

   

Wageni waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti