Balozi wa Pamba nchini Mhe. Aggrey Mwanri amewataka wakulima katika Wilaya ya Serengeti kuacha tabia ya kuchanganya pamba na mazao mengine mashambani
ameyasema hayo wakati akiongea na wananchi wa Serengeti katika kata mbalimbali alizotembelea wakati wa uhamashiji wa kilimo bora cha pamba wilayani Serengeti.
Mwanri amesema kuchanganya pamba na mazao mengine ni moja ya sababu zinazopelekea kupatikana kwa mavuno hafifu wilayani Serengeti.
"tatizo kubwa lililopo hapa Serengeti ni kuchanganya maindi,mtama na pamba katika shamba moja jambo linalileta changamoto wakati wa unyunyiziaji wa dawa kwani kila mazao hushambuliwa na wadudu tofauti" alisema Mwanri
Vilevile Mhe. Aggrey Mwanri amewataka maafisa ughani katika kata zote wilayani Serengeti kuhakikisha wanafanyia kazi maagizo yote yalinayotoka ngazi za juu kuhusa pamba ikiwa ni pamoja na kuandaa mashamba darasa kwa ajili ya kuwafundisha wananchi juu ya kilimo bora cha pamba
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Ndg. Afraha N Hassan amewataka Maafisa kilimo wote wilayani kuhakikisha wanatimiza lengo la kupewa pikipiki kuzungukia wananchi katika mashamba yao pamoja na kutoa elimu kwa wakulima hao na si vinginevyo.
Ziara ya Balozi wa pamba Mhe. Aggrey Mwanri wilayani Serengeti ni muendelezo wa ziara yake nchi kuzungukia mikoa yote inayolima pamba ambapo katika Wilaya ya Serengeti zaidi ya kata sita na vijiji 14 vimetembelewa na kupewa semina juu ya kilimo bora cha pamba kwa zaidi ya wananchi wananchi 1071.
31603 Stendi Kuu | Serengeti
Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti
Simu ya mezani: 0282985686
Simu: 0782677763
Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz
Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti