• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Malalamiko na Mrejesho |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Malengo
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha & Biashara
      • Afya
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi & Zimamoto
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mazingira & Usafishaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • MIfugo & Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Water
    • Vitengo
      • TEHAMA & Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu.
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Ripoti Mbalimbali
      • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MAHAFALI YA KIDATO CHA SITA NATTA SEKONDARI YAFANA, WAJIPANGA KUFANYA VIZURI MITIHANI YA KITAIFA

Imewekwa: April 18th, 2023

Shule ya Sekondari Natta imefanya mahafali yake ya 11 ya kidato cha sita, ambapo jumla ya wanafunzi 111 wamehitimu masomo yao.



Akizungumza na wahitimu wakati wa mahafali hayo Mgeni rasmi Mhe.Amsab  Mrimi (Mbunge wa Jimbo la Serengeti) amewapongeza wahitimu na walimu kwa juhudi kubwa walizofanya hadi kufikia hatua hiyo. Aidha, amewakumbusha wazazi na walezi wa wanafunzi kuwa na utamaduni wa kutoa motisha ama zawadi kwa walimu ili kuwapongeza na kuwatia moyo katika kazi yao njema ya ufundishaji na malezi kwa vijana wao ili shule ya Natta iendeleze utamaduni wao wa kufanya vizuri zaidi katika taaluma.


''tunapokutana katika sherehe kama hizi wakati mwingine  bebeni zawadi kwa ajili kuwapongeza   walimu ili wapate motisha ya kufanya vizuri zaidi''amesema Mrimi.


Aidha, Mhe. Amsabi ameupongeza uongozi wa shule hiyo kwa kufanya vizuri katika utawala na matokeo ya mitihani ya kitaifa ambapo kwa matokeo ya mwaka jana (2022) shule hiyo ilishika nafasi ya kwanza (1) kati ya shule 22  kimkoa na nafasi ya 11 kati ya shule 644 kitaifa.


Pia, ametoa wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha wanawanunulia vitabu watoto wao na kuwapa muda wa kutosha wa kusoma ili waweze kupata maarifa, ujuzi na wafaulu katika masomo yao. Amewataka wanafunzi hao kumtanguliza Mungu katika masomo na mitihani yao yote.


Kwa upande wake Mkuu wa shule hiyo Mr. Mwema M. Warioba, ametoa wito kwa wanafunzi hao katika kuelekea mitihani yao ya mwisho kuzingatia waliyofundishwa na kuelekezwa na walimu wao na kuhakikisha wanajitahidi na kufanya vizuri katika mtihani wao wa mwisho unaotarajiwa kuanza tarehe 02/05/2023 ''Naomba kila mmoja wenu azingatie tuliyowafundisheni na asome kwa bidii na kuhakikisha anafanya vizuri katika mitihani hii ya mwisho kama tulivyokubaliana".

‘’kwa wanafunzi watano watakaopata division one ya point 3 na 4 tutawalipia gharama za hosteli(accomodation)kwa mwaka mmoja kwa kila mmoja  akiwa chuoni. Sambamba na motisha hiyo, mimi binafsi nitatoa tiketi moja ya ndege ya kwenda na kurudi (go and return) kwa mwanafunzi aliyekuwa bora katika taaluma kwa kipindi chote BAHATI A. JUMANNE kwenda katika chuo chochote atakachopangiwa hapa nchini'' amesema Mr. Mwema.


Aidha, Mwl. Mwema ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta jumla ya Tsh. 80,000,000/= fedha ambazo zimetumika kuboresha miundombinu katika shule hiyo kwa kujenga madarasa manne kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita na kupunguza mrundikano wa wanafunzi katika vyumba vya madarasa.


Kwa upande wa wahitimu, wao wameushukuru uongozi wa shule kwa namna ilivyowajali katika kuwahudumia na kuwapa elimu bora kwa kipindi chote walichokuwa shuleni na kuahidi kufanya vizuri zaidi katika mitihani  yao ya Taifa. Pia wametoa wito kwa serikali kuisaidia shule kwa kujenga uzio katika shule hiyo kutoka na hatari mbalimbali zinazojitokeza mara kadhaa ikiwemo kuvamia na wanyama wakali pamoja na vibaka wanaohatarisha usalama wa wanafunzi na mali za umma.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI KWA WAENDESHA BVR NA WAANDISHI MSAIDIZI April 28, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU. March 07, 2025
  • TANGAZO LA KUTOA MAONI KUHUSU SHERIA NDOGO. February 24, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA January 02, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU YA MALARIA WILAYANI SERENGETI

    April 25, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO WATEMBELEA ENEO LA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    April 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SERENGETI LAPITISHA BILIONI 48.8 KAMA MPANGO WA BAJETI YA HALMASHAURI 2025/2026.

    March 04, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI WILAYANI SERENGETI LAPITISHA MPANGO WA BAJETI YA TARURA BILIONI 2.4

    March 03, 2025
  • Angalia zote

Video

AKINA MAMA SERENGETI WASEMA ASANTE MAMA SAMIA.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Maktaba ya Picha za Matukio mbali mbali
  • Matokeo ya Kidato cha nne mwaka 2017
  • Bofya hapa kupata fomu mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • UCHAGUZI KIDATO CHA KWANZA 2022 SERENGETI DC
  • FOLLOW US INSTAGRAM
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili (FTNA) 2017
  • FOLLOW US TWITTER

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Rais
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Mkoa wa MARA
  • Tanzania National Parks TANAPA
  • Frankfurt Zoological Society (FZS)

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    31603 Stendi Kuu | Serengeti

    Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti

    Simu ya mezani: 0282985686

    Simu: 0782677763

    Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz

Other Contacts

   

Wageni waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti