Kamati ya Lishe ya Halmashauri ya wilaya ya Serengeti imeazimia kuwa kila shule ihakikishe inatoa huduma ya chakula shuleni kwa wanafunzi ambapo katika robo ya Pili idadi ya shule zinazotoa huduma ya chakula shuleni imeongezeka ,aidha kamati imeagiza kila shule kuhakikisha inatekeleza agizo hilo mara Moja.
Ambapo Mzazi au Mlezi atatakiwa kuchangia Kilo nne(4) za mahindi kwa ajili ya mtoto wake awapo shuleni.
Wajumbe wa Kamati ya Lishe wakijadili na kupitia taarifa mbalimbaliz afua za lishe Mapema
wiki Hii katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Serengeti
Kikao hiki pia kilifanya tathimini ya hali lishe kwa ujumla katika wilaya ya Serengeti, Kupokea na kupitia Taarifa za utekelezaji wa Afua Mbalimbali za lishe kwa kipindi cha robo ya pili (Octoba- Disemba 2022).kikao hiki kilifanyika katika Ukumbi Wa Halmashauri.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Serengeti Ndg.Kivuma H.Msangi akifatili
kwa karibu majadiliano mbalimbali ya kuboresha afua za lishe wilayani.
31603 Stendi Kuu | Serengeti
Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti
Simu ya mezani: 0282985686
Simu: 0782677763
Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz
Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti