• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Malalamiko na Mrejesho |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Malengo
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha & Biashara
      • Afya
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi & Zimamoto
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mazingira & Usafishaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • MIfugo & Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Water
    • Vitengo
      • TEHAMA & Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu.
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Ripoti Mbalimbali
      • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Hospitali ya Wilaya sasa kukamilika Mwezi Disemba 2017.

Imewekwa: June 6th, 2017

Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Dk. Deo Kisaka (kulia) akitoa maelezo ya mchoro sanifu wa hospitali ya Wilaya ya Serengeti kwa Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 06 Juni 2017 amefanya ziara ya kikazi Wilayani Serengeti, Mkoa wa Mara.

Katika ziara hiyo Makamu wa Rais ametembelea Kijiji cha Kibeyo nje kidogo ya Mji wa Mugumu ambapo ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Serengeti unaendelea na kuweka jiwe la msingi hospitalini hapo na kisha kufanya mkutano wa hadhara katika uwanja wa mbuzi katika Mji wa Mugumu.

Hafla ya kuweka jiwe la msingi katika hospitali ya Wilaya pamoja na mkutano wa hadhara zilihudhuliwa na umati mkubwa wa watu pamoja na viongozi mbali mbali kutoka mkoa wa mara wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Dk. Charles Mlingwa.

Taarifa aliyoitoa Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Nurdin Babu kwa Makamu wa Rais, amebainisha changamoto ya ukosefu wa fedha katika kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo. “Hadi kufika mwaka 2014 jumla ya Tshs 1,859,284,000 zilikwisha tumika katika ujenzi wa hospitali, na kuanzia mwaka 2015 mpaka sasa bado hatujapata fedha kukamilisha ujenzi wa hospitali” alisema Babu. Aidha Mkuu wa Wilaya amesema Jumla ya Tshs 1,478,859,289 zinahitajika katika kukamilisha ujenzi wa majengo ya wagonjwa wa nje (OPD) katika awamu hii ya kwanza ya ujenzi na anatarajia ifikapo mwezi Disemba huduma za afya ziwe zinatolewa.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amepongeza juhudi zilizofanywa na uongozi wa Serikali, viongozi wa siasa pamoja na wadau wa maendeleo ndani ya Wilaya ya Serengeti na Mkoa wa Mara katika ujenzi wa hospitali ya Wilaya.

“Leo hii tunahimiza ujenzi wa hospitali na vyumba vya upasuaji Tanzania nzima, kweli mmefanya kazi nzuri hospitali haijaisha lakini mpaka mlipofika nimejua hapa watu wako makini. Nawapongeza kwa hatua mliyofikia” amesema Makamu wa Rais. Aidha Mhe. Samia Suluhu ameahidi kuchangia Shilingi Milioni 5 katika ujenzi wa hospitali unaoendelea huku akiahidi kusimamia ujenzi wa hospitali na kuhakikisha serikali inaleta fedha ili kukamilisha ujenzi.

Naye Mbunge wa Jimbo la Serengeti Mhe. Marwa Ryoba Chacha ameiomba serikali kuleta fedha kwa wakati ili miradi iliyokusudiwa na kuanzishwa iweze kukamilika kwa wakati. “Kukamilika kwa hospitali hii kutasaidia wananchi pamoja na watalii wanaotembelea Hifadhi yaTaifa ya Serengeti kupata huduma bora za afya ndani ya Wilaya ya Serengeti” amesema Mhe Mbunge.

Ujenzi wa hospitali ya Wilaya ulianza mnamo mwaka 2009 kupitia mkandarasi Gross Investment Ltd na kufikia mwaka 2015 ujenzi ulisimama kutokana na ukosefu wa fedha. Ziara hii ya Makamu wa Rais inaleta mwanga wa matumaini ya kukamilika kwa hospitali hiyo ifikapo mwezi Disemba 2017 na wananchi kupata huduma bora za afya ndani ya Wilaya ya Serengeti.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI KWA WAENDESHA BVR NA WAANDISHI MSAIDIZI April 28, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU. March 07, 2025
  • TANGAZO LA KUTOA MAONI KUHUSU SHERIA NDOGO. February 24, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA January 02, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU YA MALARIA WILAYANI SERENGETI

    April 25, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO WATEMBELEA ENEO LA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    April 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SERENGETI LAPITISHA BILIONI 48.8 KAMA MPANGO WA BAJETI YA HALMASHAURI 2025/2026.

    March 04, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI WILAYANI SERENGETI LAPITISHA MPANGO WA BAJETI YA TARURA BILIONI 2.4

    March 03, 2025
  • Angalia zote

Video

AKINA MAMA SERENGETI WASEMA ASANTE MAMA SAMIA.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Maktaba ya Picha za Matukio mbali mbali
  • Matokeo ya Kidato cha nne mwaka 2017
  • Bofya hapa kupata fomu mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • UCHAGUZI KIDATO CHA KWANZA 2022 SERENGETI DC
  • FOLLOW US INSTAGRAM
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili (FTNA) 2017
  • FOLLOW US TWITTER

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Rais
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Mkoa wa MARA
  • Tanzania National Parks TANAPA
  • Frankfurt Zoological Society (FZS)

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    31603 Stendi Kuu | Serengeti

    Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti

    Simu ya mezani: 0282985686

    Simu: 0782677763

    Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz

Other Contacts

   

Wageni waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti