• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Malalamiko na Mrejesho |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Malengo
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha & Biashara
      • Afya
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi & Zimamoto
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mazingira & Usafishaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • MIfugo & Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Water
    • Vitengo
      • TEHAMA & Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu.
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Ripoti Mbalimbali
      • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Fedha za Tasaf chachu ya maendeleo ya kaya masikini Serengeti.

Imewekwa: July 12th, 2018

“Zamani nilikuwa katika hali ngumu sana, nilikuwa sina chochote kile. Nawashukuru sana Tasaf kuja na mpango huu, maendeleo niliyonayo sasa ni mazuri”

Hiyo ni kauli ya mnufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini (awamu ya tatu) kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bi. Verediana Sakwe mkazi wa Kijiji cha Makundusi, Kata ya Natta wilayani Serengeti akiongelea manufaa aliyoyapata tangu kuingia kwenye mpango huo.

Bi. Verediana ambaye ni mama wa watoto wanne anasema kuwa kupitia fedha alizokuwa anapata kutoka Tasaf amefanikiwa kuanzisha mradi wa ufugaji kondoo pamoja na biashara ya mahindi. Katika shughuli ya ufugaji alianza na kondoo wawili huku akiishi katika nyumba yake ya awali (nyumba ya tembe) ambayo aliibomoa baada ya kuanza kunufaika na miradi aliyoanzisha.

Bi. Verediana akichunga mifugo yake (kondoo) jirani ya nyumbani kwake, kijijini Makundusi.

“Nilianza kuwa kufuga kondoo wawili huku nikiishi katika nyumba ya tope, niliendelea na hali hiyo mpaka nilipokusanya fedha za kutosha kujenga nyumba yangu hii mpya ta tofali za kuchoma” anasema Bi. Verediana. Huku akiendelea kwa kusema namshukuru mungu kwa sasa naendelea vizuri nina kondoo 20 na naendela na biashara”

Bi. Verediana akitoka kwenye nyumba aliyojenga kutokana na matunda ya fedha za Tasaf.

Naye Bi. Chausiku Tareta mkazi wa kijijini hapo amefurahishwa na mpango huo kutokana na matunda anayoyapata kupitia fedha za Tasaf. “Nilikuwa nafanya biashara ya mbogamboga na kufanikiwa kupata faida ya shilingi elfu kumi ambayo niliitumia kuanzisha biashara ya kuuza supu” Bi. Tareta akielezea hali aliyokuwa nayo kabla ya kuingia kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini. Kupitia fedha za Tasaf Bi. Tareta amekuza biashara yake na sasa ana duka la vitu vya reja reja huku akiishukuru Tasaf kwa kumkwamua katika umasikini.

Licha ya kuanzisha biashara mpya Bi. Tareta bado anaendelea kuuza supu inayopatikana pembeni kidogo ya duka lake “Kwa sasa nauza vitu hapa dukani lakini pia naendela na kazi yangu ya kuuza supu, nawashukuru sana Tasaf kwa kunisaidia”

Bi. Tareta mkazi wa Kijiji cha Makundusi, Kata ya Natta akionyesha biashara ya duka aliloanzisha kutokana na fedha za Tasaf.

Toka kuanza kwa mpango huo Mwezi Julai mwaka 2015 jumla ya shilingi Bilioni 2.6 za kitanzania zimetumika kuwanufaisha walengwa kwa kaya 3,666 za Wilaya ya Serengeti. Aidha kaya 228 zimeondolewa kutokana na sababu za kukosa sifa kuendelea kuwa kwenye mpango na kufanya kaya zilizosalia kwenue mpango kuwa 3,438. Anasema Mratibu wa mpango wa kunusuru kaya masikini awamu ya tatu (3) Bi. Antusa Swai.

Akitaja sababu za kukosa sifa, Mshauri wa mpango huo Bwana Sokoro Munubi amezitaja sababu zinazisababisha wajumbe kukosa sifa ni; wajumbe kuhama makazi walioandikishiwa, kufariki pamoja na wanufaika kutokwenda kuchukua fedha mara tatu mfululizo hivyo kusababisha kuondolewa kwenye mpango.

Licha ya kutolewa kwa fedha hizo kwa kaya masikini ili kuboresha hali za maisha na kuanzisha miradi mbalimbali, bado kuna changamoto ya walengwa kutotumia fedha hizo kwa matumizi yaliyokusudiwa huku baadhi yao wakiwa katika hali zile zile kabla ya kuingia kwenye mpango.

Bi. Antusa Swai anakiri kuwepo kwa changamoto hiyo na ofisi ya Tasaf wilayani kwa kushirikiana na maafisa wa maendeleo ya jamii ngazi ya Kata wamekuwa wakishirikiana katika kutoa elimu ya ujasiliamali ili kaya ziweze kuanzisha miradi itakayowaingizia kipato. “Huwa tunatoa elimu ya ujasiliamali kupitia maafisa ugani waliopo ngazi ya Kata na Vijiji lakini pia wakati wa malipo huwa tunawaelimisha walengwa kuanzisha miradi itakayokuwa inawaingia kipato” anasema Bi. Antusa Swai.

Mpango wa kunusuru kaya masikini unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika Wilaya ya Serengeti ulianza kuwanufaisha walengwa waliohakikiwa kupitia uchunguzi na uliofanywa na wataalam na kupitishwa na vikao ngazi za vitongoji na vijiji ili kuwabaini walengwa halali waliostahili kupatiwa misaada.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI KWA WAENDESHA BVR NA WAANDISHI MSAIDIZI April 28, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU. March 07, 2025
  • TANGAZO LA KUTOA MAONI KUHUSU SHERIA NDOGO. February 24, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA January 02, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU YA MALARIA WILAYANI SERENGETI

    April 25, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO WATEMBELEA ENEO LA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    April 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SERENGETI LAPITISHA BILIONI 48.8 KAMA MPANGO WA BAJETI YA HALMASHAURI 2025/2026.

    March 04, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI WILAYANI SERENGETI LAPITISHA MPANGO WA BAJETI YA TARURA BILIONI 2.4

    March 03, 2025
  • Angalia zote

Video

AKINA MAMA SERENGETI WASEMA ASANTE MAMA SAMIA.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Maktaba ya Picha za Matukio mbali mbali
  • Matokeo ya Kidato cha nne mwaka 2017
  • Bofya hapa kupata fomu mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • UCHAGUZI KIDATO CHA KWANZA 2022 SERENGETI DC
  • FOLLOW US INSTAGRAM
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili (FTNA) 2017
  • FOLLOW US TWITTER

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Rais
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Mkoa wa MARA
  • Tanzania National Parks TANAPA
  • Frankfurt Zoological Society (FZS)

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    31603 Stendi Kuu | Serengeti

    Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti

    Simu ya mezani: 0282985686

    Simu: 0782677763

    Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz

Other Contacts

   

Wageni waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti