• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Malalamiko na Mrejesho |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Malengo
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha & Biashara
      • Afya
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi & Zimamoto
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mazingira & Usafishaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • MIfugo & Uvuvi
      • Ardhi & Maliasili
      • Water
    • Vitengo
      • TEHAMA & Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Water
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu.
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Ripoti Mbalimbali
      • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Agizo la Mheshimiwa Majaliwa kwa watumishi wa Idara ya afya Serengeti.

Imewekwa: January 19th, 2018

Watumishi wa idara ya afya katika Wilaya ya Serengeti wametakiwa kutoa bure huduma za matibabu kwa wazee wenye miaka zaidi ya 60 walio na vitambulisho.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa akitoa kitambusho kwa Mzee johannes Magaigwa Chacha.

Agizo hilo limetolewa na jana tarehe 18 Januari 2018 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa alipokuwa akikabidhi vitambulisho 280 kwa wazee ili kupatiwa huduma za matibabu popote katika zahanati, vituo vya afya na hospitali ndani ya Wilaya ya Serengeti.

“Nawapongeza Serengeti kwa kutekeleza kwa vitendo agizo hili la Rais, Mheshimiwa Magufuli la kutaka wazee wenye umri kuanzia miaka 60 watibiwe bure” alisema Mheshimwia Majaliwa na kuendelea kwa kusema “Natoa agizo kwa watumishi wa afya kuwahudumia bure wazee wenye vitambulisho hivi na msiwatoze  fedha yoyote”

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa akikagua ujenzi wa hospitali ya WIlaya Serengeti.

Awali Mheshimiwa Majaliwa alipata nafasi ya kukagua mradi wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya inayojengwa katika eneo la Kibeyo nje kidogo ya Mji wa Mugumu Serengeti na kupokea taarifa ya ujenzi wa hospitali hiyo toka kwa Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mheshimiwa Nurdin Babu.

“Kwa muda mrefu sasa ujenzi wa Hospitali ulikuwa umesimama, kwa kushirikiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Mhandisi Juma Hamsini, tuliunda kamati maalumu iliyohusika na uhamsishaji wa ujenzi wa hospitali hii na kupitia kampeni ya Jenga Hospitali kwa shilingi elfu moja (1000) pamoja na kufanya harambee tumepata fedha za ujenzi wa hospitali hii mpaka hatua hii unayoiona sasa”

Waziri Mkuu alionyesha kuguswa na jitihada za ukamilisahji wa Hospitali hiyo na kuahidi kuchangia kiasi cha shilingi milioni 10 za kitanzania kuunga mkono. Aidha katika harambee iliyofanyika hospitalini hapo raia mwema mwenye mapenzi na Wilaya ya Serengeti Bwana Adrea nyantori alitoa fedha taslimu shilingi milioni kumi papo hapo kuunga mkono huku jumla ya shilingi milioni thelathini na moja na elfu hamsini (31,050,000/=) zilichangwa pamoja na ahadi za mifuko mia sita na tano (605) ya saruji kutoka kwa wadau wa maendeleo.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa akipokea fedha taslimu kiasi cha shilingi milioni 10 (mchango wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Serengeti) toka kwa Bwana Andrea Nyantori.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa akiteta jambo na Bwana Andrea Nyantori.

Mheshimwa Babu hakusita kumuomba Mheshimwa Majaliwa kuisaidia Wilaya ya Serengeti kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo kwa kuipigia chapuo ili iweze kupatiwa fedha na Serikali kuu huku akitarajia huduma kuanza kutolewa mwishoni mwa mwezi februari mwaka 2018.

Kaimu Mganga mkuu Wilaya ya Serengeti Daktari Deo Kisaka akimuonyesha Mheshimiwa Majaliwa mchoro sanifu wa hospitali ya Wilaya ya Serengeti


Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI KWA WAENDESHA BVR NA WAANDISHI MSAIDIZI April 28, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU. March 07, 2025
  • TANGAZO LA KUTOA MAONI KUHUSU SHERIA NDOGO. February 24, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA January 02, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU YA MALARIA WILAYANI SERENGETI

    April 25, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO WATEMBELEA ENEO LA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    April 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SERENGETI LAPITISHA BILIONI 48.8 KAMA MPANGO WA BAJETI YA HALMASHAURI 2025/2026.

    March 04, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI WILAYANI SERENGETI LAPITISHA MPANGO WA BAJETI YA TARURA BILIONI 2.4

    March 03, 2025
  • Angalia zote

Video

AKINA MAMA SERENGETI WASEMA ASANTE MAMA SAMIA.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Maktaba ya Picha za Matukio mbali mbali
  • Matokeo ya Kidato cha nne mwaka 2017
  • Bofya hapa kupata fomu mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • UCHAGUZI KIDATO CHA KWANZA 2022 SERENGETI DC
  • FOLLOW US INSTAGRAM
  • Matokeo ya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha pili (FTNA) 2017
  • FOLLOW US TWITTER

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu ya Rais
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Mkoa wa MARA
  • Tanzania National Parks TANAPA
  • Frankfurt Zoological Society (FZS)

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    31603 Stendi Kuu | Serengeti

    Anuani ya Posta: 176 Mugumu Serengeti

    Simu ya mezani: 0282985686

    Simu: 0782677763

    Barua pepe: ded@serengetidc.go.tz

Other Contacts

   

Wageni waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki © 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti